Recents in Beach

header ads

BABA P...BABA PILI...BABA PILIMA! - 1




Chombezo : Baba P...Baba Pili...Baba Pilima! 
Sehemu Ya Kwanza (1)


Samahani kaka, sijui hiki kiti kina mtu?” aliuliza Kate au maarufu kwa jina la mama Pilima!
Ilikuwa kwenye baa ya Dolphin, iliyopo kwenye Jiji la Tanga maeneo ya Kwaminchi…
“Hapana anti, unaweza kuchukua tu maana aliyekaa ameshaondoka,” alijibu mwanaume mmoja aliyekutwa amekaa kwenye kiti pembeni ya meza hiyo.
Mama Pilima alikichukua kiti hicho na kuanza kutafuta meza nyingine tupu ili akae lakini akaikosa, akarudi na kiti mpaka kwenye meza hiyo kwa sababu mwanaume huyo alikaa peke yake…
“Samahani tena! Naweza kukaa hapa!”
“Unaweza kukaa tu maana hakuna mtu mwingine atakayekuja kukaa.”
Mama Pilima aliweka kiti hapo na kukaa kisha akaangalia upande walipokaa wahudumu lakini kwa bahati, mhudumu mmoja alisimama nyuma yake akisubiri akae ili amsikilize…
“Anti naomba bia ya baridi sana.”
“Bia gani?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Ooo! Lete Mount Meru.”
Wakati mhudumu ameondoka, mama Pilima alimgeukia yule mwanamke huku akijipepea kwa kitambaa kupunguza jasho…
“Samahani kwa usumbufu lakini,” alisema mama Pilima.
“Wala usijali,” alisema yule mwanaume huku akimwangalia mama Pilima kwa macho ya kumtathmini. Kila jicho lake lilipotua, ilikuwa moyoni akis ema, ‘lakini umeumbwa! Utakuwa umeolewa kweli wewe? Mbona kama nimevutika na wewe!’
Na mama Pilima naye alipokutana macho na mwanaume huyo alimwangalia kama anayesema, ‘ukinitongoza nitakubali, lakini siwezi kukuanza maana naona unanitamani sana.’
Wakati wawili hao kila mmoja akimuwaza mwenzake kufuatia kumtamani kimahaba bia ililetwa.
Mama Pilima aliimimina yote kwenye glasi kubwa maana alikuwa na kiu sana. Aliipiga yote kwa mpigo huku macho yakiwa kwa mhudumu kama anayesema, ‘usiende sasa, si unaona namaliza hii.’
“Nikuongeze anti?” mhudumu alimuuliza kwa sauti iliyojaa mshangao mkubwa. Mama Pilima alikubali kwa kutingisha kichwa.
Hata hivyo, kuondoa usumbufu alimwambia amletee mbili kabisa.
“Du! Kweli wanawake wengine ni balaa… yaani huyu dada kaikata bia yote tena ya baridi bila kupumzika? Hii ni hatari!” yule mduhumu aliwaza.
Mhudumu alipoondoka, mama Pilima akamwangalia yule mwanaume na kusema…
“Sikukeri?”
“Wala!”
“Basi nashukuru sana…maana kuna watu wakikaa kwenye meza kama hivi wanapenda kukaa wenyewe tu.”
“Mimi wala,” alirudia kusema yule mwanaume…
“Oke, mimi naitwa Keti au mama Pilima…mwenzangu?” alianza kujitambulisha mama Pilima hata bila ya kuombwa…
“He! Kweli ndiyo jina lako?” alishtuka yule mwanaume…
“Ndiyo! Kwani vipi?”
“Mimi mke wangu pia anaitwa Keti lakini yeye ni mama Pili…”
“Mh! Hayo kweli maajabu! Ilikuajekuaje mpaka kufanana majina yetu na ya watoto?” aliuliza mama Pilima…
“Ndiyo nashangaa.”
“Kwa hiyo wewe ni baba Pili..?”
“Eee baba Pili!”
“Unaitwa nani ukiachana na jina la mwanao la baba fulani..?”
“Mimi naitwa Sam…”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Hamna bwana,” alisema yule mwanamke huku akisimama na kuweka glasi ya bia mezani…
“Hamna nini sasa?”
“Yaani mimi nifanane majina na mkeo, wewe ufanane na mume wangu! Inawezekana kweli?”
“Kwani mumeo naye anaitwa Sam?”
“Eee! Ndiyo nashangaa hapa…”
“Mh! Hiyo kweli kali. Si ajabu hata makabila mimi na mumeo ni sawa?”
“Inawezekana baba Pili. Wewe kabisa gani?”
“Natoka Mkoa wa Dodoma…”
“Unaona sasa baba Pili…na mimi Sam mwenzako anatoka mkoa huohuo? Mkeo je?”
Baba Pili aliachia tabasamu na kusema…
“Aaa! Haiwezekani na wewe ukafanana kabila na mke wangu bwana. Itakuwa too much sasa!”
“We nitajie…wewe unatoka Mkoa wa Dodoma, mume wangu pia hukohuko. Je mkeo anatokea mkoa gani?”
“Yeye mke wangu anatokea Mkoa wa Dodoma pia…”
“Noo! Noo! Napingana na wewe baba Pili. Kinachoonekana hapa kuna kitu unakitengeneza…”
“Kwa nini? Kwani mimi nakujua wewe?”
“Inawezekana unanijua kiroho au kimwili,” alisema mama Pilima akiwa amesimama bado tangu aseme zile noo zake!
“Mimi sijawahi kukuona hata siku moja. Lakini jua Mungu ana makusudi yake mama Pilima. We fikiria ni kwa nini ulikuja kuomba kiti kwangu? Halafu ukakosa pa kukiweka ukaja kukiweka hapahapa ulipokitoa?”
“Asee kweli kabisa baba Pili. Hapa nadhani pana neno tunaambiwa,” alisema mama Pilima…
“Eee! Nyie mnaishi wapi?” aliuliza baba Pili…
“Magomeni Kagera…”
“Ah! Nimechoka sana jamani…”
“Kwa nini?”
“Sisi tunaishi Magomeni Mwembechai!”
“He! Kwa hiyo wote ni Magomeni?”
“Ndiyo maana yake.”
“Watoto wako wanasoma wapi?”
“Watoto mtoto? Mimi nina mtoto huyohuyo mmoja tu…”
“Aaa! Noo bwana…nooo!”
http://deusdeditmahunda.blogspot.com/


Mhudumu alitokea na kuingilia mazungumzo yao kwa kumuuliza baba Pili kama anataka kuongezea kinywaji…
“Tuongezee tafadhali,” alisema baba Pili…
Baada ya mhudumu kuondoka, waliendelea…
“Ina maana tunaweza kufanana kwa kila kitu kiasi hicho?” aliuliza baba Pili…
“Na mimi ndiyo nashangaa,” alijibu mama Pilima…
“Mh! Yaani hadi eneo la kuishi, yaani wote Magomeni?”
“Ndiyo hapo sasa.”
Moyoni baba Pili aliamini ile ndo’ ilikuwa fursa pekee ya kumnasa mwanamke huyo aliyeonekana kwake ana mvuto…
“Lakini kama mwingi wa habari…maana ukiona mwanamke unaongea naye na anakukodolea macho bila kufumbafumba, ogopa,” alijisemea moyoni mwanaume huyo.
Sasa wakawa kama marafiki waliojuana siku au miaka mingi sana. Walipiga stori nyingine za kifamilia na za nje ya familia. Za kifamilia zilikuwa hizi…
“Sasa mama Pilima, kama kuna baba Pilima unawezaje kutoka kukaa baa peke yako?” aliuliza baba Pili…
“Ah! Unajua ukifanya utafiti utagundua kuwa, wanaopenda kulewa, katika kila watu kumi, sita wana stresi zao, wanne tu ndiyo wanakwenda kwa matakwa yao…”
“Sasa wewe mama Pilima upo kundi gani?”
“La watu sita…teh! Teh! Teh!” alijibu mama Pilima na kucheka kidogo…
“Una stresi?”
“Ndiyo maana yake!”
“Zaidi ni nini?”
“Ah! Unajua tena mambo ya ndoa baba Pili…”
“Yamefanyaje?”
Mama Pilima akaachia tabasamu kidogo kisha akamwangalia baba Pili kwa macho ya mlegezo…
“Mambo ya aibu bwana,” alisema mama Pilima…http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mh! Sisi wanandoa hatuna mambo ya aibu. Labda kama tungekuwa mabachela…teh! Teh! Teh!”
Mama Pilima aliamua kuachia ukweli kama kawaida ya wanawake…
“Unajua mimi na mume wangu, hata kuzaa ni kama Mungu tu…”
“Kwa nini iwe kama Mungu tu…”
“Ah! Yaani ningejua…wala…”
“Nini tena jamani mama Pilima?”
“Unajua mimi nilifunga ndoa bila kukutana kimwili na mume wangu…”
“Enhee..?”
“Tukiwa honeymoon ndiyo nikabaini tatizo…”
“Tatizo gani mama Pilima?” aliuliza baba Pili macho yote yakiwa kwenye uso wa mwanamke huyo ambaye katika kuongea alikuwa akibinua midomo, mara alegeze macho, mara aachie tabasamu la huba. Ilimradi tu!
“Nilishangaa sana, mume wangu alipoanza tu palepale akamaliza. Na mbaya zaidi akimaliza hawezi kuendelea tena mpaka upite mwezi na siku kadhaa…”
“Lo! Kweli hilo tatizo mama Pilima…”
“Umeona ee?”
“Basi bora angekuwa anasubiri hata dakika mbili, yaani yeye ni sekunde saba tu.”
“Sekunde saba!” alishangaa baba Pili…
“Ndiyo sekunde saba…siku nyingine hata kabla ya kuanza kwa mechi.”
Hapo baba Pili alijikuta akiangalia pembeni kwa aibu. Maana alimwona mama Pilima kama ameenda ndani sana. Halafu na yeye na vile alishamtamani, ikawa kwake ni kama anapunguziwa kazi…
“Lo! Kwa hiyo unahisi kulewa ndiyo sababu ya kukufanya uweje?”
Kwa kweli nikilewa, nikifika nalala zangu tu…teh Teh! Lakini nisipolewa, da! Namsumbua nikijua wazi kwamba, atanitesa tu.”
“Mimi naomba kukushauri,” alisema baba Pili. Mama Pilima akakaa mkao wa kusikiliza kwa undani zaidi…
“Enhe! Nasikiliza wazo lako baba Pili…”
“Badala ya kunywa pombe mpaka kulewa, ungetafuta wa pembeni ili awe mkata kiu yako,” alisema baba Pili huku akiangalia chini. Alijua si ushauri mzuri lakini kwa sababu yeye anafukuzia mzigo ilibidi aseme hivyo ili apime!http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mh,” aliguna mama Pilima huku na yeye akiangalia upande mwingine kwa walipokuwa wamekaa wahudumu…
“Nimekukwaza kwa ushauri wangu mama Pilima?”
“Kwa kiasi fulani umenikwaza sana…”
“Kwa nini?”
“Sijawahi kusaliti na wala sipendi. Ingawa kama mwanamke naweza nikawa katika hali ya kujisikia kufanya hivyo lakini huwa najionya.”
Baba Pili alihema kwa nguvu na kumwangalia mwanamke huyo kisha akasema…



ITAENDELEA

Post a Comment

0 Comments