Recents in Beach

header ads

BABA P...BABA PILI...BABA PILIMA! - 2



Chombezo : Baba P...Baba Pili...Baba Pilima! 
Sehemu Ya Pili (2)


“Unafikiri unaweza kukaa hivyo kwa kipindi gani?’ aliuliza baba Pili.
“Kwa kipindi kirefu lakini kumsaliti mume wangu naona ngumu sana,” alisema mama Pilima, kwa kumwangalia tu ungegundua kwamba aliamua kukaza kidogo, yaani kama gari, lilijifanya kutowaka ili litekenywe zaidi…http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kwani kuna ubaya gani kama utatafuta kitu cha kukuridhisha hasa unapoona hauridhiki? Mama Pilima, tafuta haki yako, kufikishwa unapotaka kufika ndiyo kitu cha msingi kwenye mwili wako,” alisema baba Pili, sasa aliamua kumkazia macho mwanamke huyo, macho yenye kuelezea hisia zote za kimapenzi….
“Jamani mimi naogopa, atajua tu,” alisema mama Pilima….
“Atajuaje sasa? Au utamwambia?”
“Nimwambie! Sijitaki!”
“Sasa atajuaje? Hiyo itakuwa siri yako wewe na huyo mtu, yaani mtakuwa mkipiga shoo kimyakimya, hata majirani hawatajua,” alisema baba Pili….
Mama Pilima akanyamaza, alimwangalia baba Pili kwa macho ya kuita, yaliyolegea kama nyanya, alijitahidi kuyarembua kwa ishara ya kumwambia baba Pili, ‘sasa inakuwaje? Upo fiti nikupe chansi?’
Baba Pili alikuwa na mawazo yake, alichokifikiria kichwani mwake kilikuwa ni kumtega mwanamke huyo, kwanza ajue kama alikuwa mwepesi au laini.
Alishaanza kuchombeza, mifano mingi ya kumwambia amchukue mwanaume yeyote pasipo kujiweka wazi kwamba alitaka huyo mwanaume awe yeye.
“Kwa hiyo?” aliuliza baba Pili mara baada ya kupita ukimya kidogo.
“Ndiyo najifikiria hivyo mwenzio…”
“Jifikirie basi halafu chukua maamuzi, kila mwanamke anataka kuridhishwa bwana…” alisema baba Pili.
Waliendelea kuzungumza kwa muda huku taratibu wakiendelea kunywa pombe zao, walipomaliza, wakaagana tayari kwa kuondoka.
“Jamani! Kwa hiyo ndiyo basi hivyo?” aliuliza baba Pili.
“Kivipi tena?”
“Hata namba ya simu, sasa tutawasiliana vipi baada ya hapa?”
Mmh! Aya, subiri nikupe, andika..” alisema mama Pilima, hapohapo akampa namba ya simu baba Pili kisha kuondoka.
Njiani, baba Pili alichanganyikiwa, akawa hoi, mama Pilima alimuweka kwenye wakati mgumu, kwa kumwangalia tu, alionekana kuwa mwanamke mtundu sana kwenye sita kwa sita, kichwa chake kilimfikiria sana.
Kwa upande wa mama Pilima sasa, alipagawa, akasahau kama alikuwa mke wa mtu, mwanaume aliyekutana naye baa, alimuweka njia panda. Kiukweli hakutaka kabisa kumsaliti mumewe lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea, alishindwa kuvumilia.
“Kwa hiyo? Jitahidi tu, hatajua,” mama Pilima alisikia sauti ya baba Pili kichwani mwake.
“Nitajaribu…” alijikuta akiongea kwa sauti.
Wakati akifikiria hayo, ghafla simu yake ikatoa mlio wa kumjulisha kwamba kuna meseji ilikuwa imeingia, hapohapo akaifungua, alipoliona jina la baba Pili, akahisi mapigo yake ya moyo yakidunda kwa nguvu.
“Umefika?” iliuliza, harakaharaka akajibu…
“Ndiyo, nimejifungia chumbani tu, mpweke kweli…”
“Kwani baba Pilima hayupo?”
“Hayupo, amekwenda kuchukua mizigo yake ya ofisini, aliniambia kwamba kesho anasafiri, anakwenda Tanga kikazi, atakaa kwa wiki moja, hapa ndiyo nimechanganyikiwa, sijui itakuwaje,” aliandika mama Pilima.
Baba Pili hakutaka kuvumilia kuchati tu kwenye simu, alijiona anachelewa, hapohapo akamtwangia, alitaka kuzungumza naye zaidi.
“Umesemaje vile?” aliuliza baba Pili.
“Mume wangu anasafiri kesho…”
“Kweli?”
“Ndiyo! Sasa sijui itakuwaje…”
“Kwani huyo mtu umeshampata? Au mpaka umtafute?” aliuliza baba Pili.
“Bado…yaani sijui nitampata wapi! Kwanza najua leo hapa huyu mzee sijui kama atanipa haki yangu, na hata akinipa, sitaridhiki mie…” alisema mama Pilima kwa sauti ya kulalamika.
“Mmmh! Kwa hiyo itakuwaje? Au tuonane sehemu tulizungumzie hilo…”
“Lini?”
“Kesho.”
“Saa ngapi?”
“Muda wowote…yaani mimi nipo free, siendi popote pale, yaani popote pale sitokwenda,” alisema baba Pili, alisisitiza zaidi ili aonekane kweli alikuwa free.
“Basi tutapanga tuone inakuwaje…”
“Sawa..nimekuelewa, ninatamani sana nikuone, tena nimekumisi mno….” alisema baba Pili.
“Mmh! Yaani kipindi kifupi hiki umenimisi?”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Ndiyo! Niliipenda sana kampani yako, umechangamka sana, unapendeza na unajua kuzungumza na mwanaume, naamini baba Pilima anafaidi sana dodo…” alisema baba Pili na mama Pilima akatoa kicheko kilichomwambia baba Pili, ‘na wewe unataka kula dodo? Basi karibu sisi twala…’



Mama Pilima alifika nyumbani akiwa mchangamfu hasa baada ya kukutana na baba Pili. Aliamini ameingiza kitu kipya katika maisha yake ya siku hiyo.
Aliweka simu juu ya meza, wifi yake anaitwa Sonia, alikuwa amekaa sebuleni. Mama Pili alikwenda chooni.
Baba Pili alipofika nje ya nyumba yake, aliamua kumpigia simu mama Pilima halafu ndiyo aingie ndani…
“Ngoja nimcheki huyu kwa simu kwanza ndiyo niingie, sijui kafika salama? Yaani bonge la demu ila hajijui tu…mtu kaumbwa utadhani kilitumika kiwanda…mimi yale macho yake du…halafu ana mwanya f’lani hivi…lakini saa zile alipoinuka kwenda toileti ndiyo nikamkubali.
“Ile ndiyo shepu bwana! Kabinuka halafu katikati pameingia…kwa kweli ni demu bomba kama nitampata lazima awe nyumba ndogo yangu…”
Simu ya mama Pilima iliita, wifi yake Sonia akainuka kuangalia anayepiga…
“Wifi…” aliita kwa sauti…
“Bee…”
“Kaka anapiga,” alisema Sonia baada ya kuona jina la baba Pili kwenye skrini.
Mama Pilima alitoka mbio akijua kweli ni mume wake…
“Mh!” aliguna kwanza alipoona jina la baba Pili…
“Eee…niambie…” alisema huku akienda chumbani…
“Ndiyo nimefika salama bwana…wewe je? Ahaaa! Sawasawa…”
Wakati mama Pilima anaendelea kuongea kwa simu huku akiingia chumbani, wifi yake alishangaa kumwona kaka yake baba Pilima anaingia…
”Khaa! Sasa wifi anaongea na nani? Mbona kaka kafika yeye bado anaongea chumbani?” alijiuliza…
“Shikamoo kaka…”
“Marhaba za hapa?”
“Njema…pole na kazi…”
“Nimepoa.”
“Wifi yako yuko wapi?”
“Nadhani chumbani.”
Baba Pili alinyoosha chumbani. Mkewe, alipoona mlango unasukumwa, alikata simu kwani alijua anayeingia bila hodi chumbani kwake ni mume wake tu.
Baada ya salamu, mama Pilima alitoka sebuleni na simu, akakaa kwenye sofa na kuanza kuchati…
“Nimepanda sauti yako baba Pili…la! mama Pili anafaidi sana hiyo sauti. Sijui unaitoaga kila mahali…!”
“Teh! Teh! Wewe acha maneno…si wewe mwenyewe unaogopa kuifaidi,” alijibu baba Pili…
“Wala siogopi, mwenzi sijawahi kusaliti. Ni hilo tu…kama ingetokea siku moja nimewahi kufanya hivyo hapo sawa, ningekuwa na uzoefu,” alijibu mama Pilima.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Walichati mengi sana, walichati mpaka sasa ikawa mama Pili anaandaa chakula huku akiwa anachati, yaani na simu mkononi. Akawa anaonekana akicheka, mara akitabasamu, mara akionekana kukazia macho simu…
***
Siku iliyofuata, mama Pilima alikwenda kwenye shughuli zake, alipomaliza jioni akiwa anarudi nyumbani kwake, alimkumbuka baba Pili…
“Si ajabu hata leo yuko pale pa jana…ngoja nimpigie,” alisema moyoni huku akiweka simu sikioni…
“Niambie mama Pilima,” alipokea baba Pili…
“Wapi?”
“Pana jana…”
“Ah! Nakuja…niagizie nusu rosti na ndizi moja…nakuja,” alisema mama Pilima…
“Sawa mama Pilima.”
Baada ya nusu saa, mama Pilima aliwasili. Alipofika, alimsogelea baba Pili, akambusu…
“Mmmwaaa…mmwaaa.”
“Da! Asante sana mama Pilima, nimejihisi nipo peponi leo. Nakupenda sana,” alisema baba Pili…
“Nakupenda pia baba Pili,” alijibu mama Pilima huku akivuta kiti na kukaa.
Walianza kuongea, wakaongea sana mambo yao. Ilifika mahali baba Pili akaanza kukumbushia ya jana yake…
“Vipi mama Pilima, bado una msimamo uleule?” aliuliza baba Pili…
“Da! Baba Pili unajua nikwambie kutoka moyoni kwamba mimi sijawahi kusaliti hata siku hii…moja! Sasa leo hii nikisema nijaribu huoni kuwa, siku ikitokea umenimwaga nitaanza kutafuta wanaume wengine, mwisho wake nitakuwa malaya…”
“Mh! Mimi mpango wangu ni kukufanya uwe nyumba ndogo yangu,” alisema baba Pili, mama Pilima akacheka sana…
“Sasa niwe nyumba ndogo yako baba Pili si utakuwa unapata shida? Mimi najua nyumba ndogo lazima iwe free…ukitaka kwenda unakwenda muda wowote ule.”
“Hapana si lazima…unaweza kuwa mke wa mtu halafu bado ukawa nyumba ndogo yangu,” alifafanua baba Pili akionekana yuko siriasi kabisa na maneno yake…


“Mh! Mimi nadhani au napendekeza tuendelee kuwa kama hivi…marafiki wakubwa lakini wa siri…mume wangu baba Pilima asijue wala mke wako mama Pili asijue…tutafurahi sana,” alisema mama Pilima huku akionekana kuachia tabasamu la mbali sana.
Hapo bia zilikuwa zikimiminika mezani. Ilifika wakati walianza vituko wakiwa wamekaa, mama Pilima alimkanyaga baba Pili, naye baba Pili akamkanyaga mama Pilima, wakaangaliana, wakachekea ndani kwa ndani, mama Pilima akamsogelea baba Pili, akatoa ulimi kuelekea kwake, baba Pili akaudaka…
Waligugumia, mihemko ilitawala, baba Pili akapeleka mkono kwenye kifua cha mama Pilima maana eneo hilo la baa walilokaa lilikuwa halina watu hata kidogo.
Kumbe mkono wa baba Pili kwenye kifua cha mama Pilima ulifanikiwa kushika nido za mwanamke huyo, akashtuka kwa maumivu ya mahaba. Ilimpa picha baba Pili kwamba, udhaifu wa mapenzi wa mama Pilima upo kifuani, akautoa mkono maana alijua kweli si mahali pake, pale ni baa.
Mama Pilima kuona amegundulika udhaifu wake, naye akawa anautafuta udhaifu wa mwanaume huyo, akapeleka mkono kifuani na kuchezea ‘bustani’ ya hapo lakini baba Pilima wala!
Akautoa mkono hapo, akamshika shingoni, wala! Akaupeleka mkono mgongoni, wala! Akaushusha, baba Pilima akalainika sana lakini hakushtuka kama alivyoshtuka yeye mama Pilima alipoguswa nido.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mama Pilima akajua kumbe udhaifu wa mwanaume huyo upo huko, akatoka na kushika glasi ya bia lakini hakuipeleka kinywani, aliendelea kubakiza ulimi wake ndani ya kinywa cha baba Pili huku akisikika kwa sauti ya…
“Mmm…mmm…mmm!”
Waliachana kwenye denda baada ya miguu ya mhudumu kutembea kuelekea walipokaa…
“Niongeze?” aliuliza mhudumu.
Mama Pilima alishika chupa ya bia ya baba Pili, akaitingisha, akaiweka chini, akashika ya kwake, akaitingisha, akaiweka chini…
“Ongeza kwa bili yangu tafadhali,” alisema.
Mhudumu alipoondoka tu, mama Pilima akaanza, akapeleka mkono kulekule alikogundua ndiko kwenye udhaifu wa baba Pili. Safari hii akaonesha hana mpango wa kuutoa haraka.
Huku akiangalia upande atakaotokea mhudumu, mama Pilima alifanya yake huku baba Pili akisinzia kwa starehe. Na vile alikuwa tayari yuko vizuri, looo!
Hali ya baba Pili ilimnasa hata mama Pilima mwenyewe aliyekuwa akisababisha. Naye akawa anaguna, anagugumia, anahemuka na anasinzia.
Kuna wakati wote walijikuta wamesinzia lakini mkono wa mama Pilima ukiwa bado kazini. Wakashtuka mhudumu alipoweka chupa za bia mezani kwa kuliza puu!
Mama Pilima ili asionekane alikuwa anafanya jambo baya, aliendelea kuuacha mkono kule…
“Fungua chapuchapu!” alisema.
Mhudumu alifungua, lakini alijua nini kilikuwa kinaendelea kwenye meza ile.
Baada ya mhudumu kuondoka, mama Pilima akakazana, baba Pili akahisi anaonewa, naye akarudia kwenye udhaifu wa mama Pilima. Sasa wakakaa kwa kuangaliana, mama Pilima kule, baba Pili pale. Walisisimka, wakashindwa kuvumilia hivyo, waliamua kuacha kwa mama Pilima kutoa kauli…
“Basi bwana! Tunakwenda kubaya,” alisema kwa sauti ya kukatakata ikitoka nje kwa njia ya puani.
Mama Pilima alivuta pumzi kwa nguvu, akazishusha huku akimwangalia baba Pili bila kusema lolote.
Baada ya hapo, waliendelea kunywa bila kusemezana, ilionekana kila mmoja alikuwa akiwaza yake moyoni kuhusu walikofikia awali.
Muda wa kufunga baa ulifika, mhudumu alikwenda kuchukua pesa yake, akalipwa! Wawili hao waliondoka huku wakiyumbayumba, wakashikana mikono ili kusaidiana kutembea.
Mama Pilima hakuwa na usafiri, baba Pili alikuwa nao, akampakia mwanamke huyo katika hali ya uleviulevi…
Baba Pili yeye ni mzima akiwa barabarani, aliendesha gari hadi Magomeni Kagera, akamshtua mama Pilima…
“Oho! Twende hadi mbele, kata kushoto, mbele utasimama. Baba Pili akafanya hivyo.
Walifika eneo la kusimama, gari likasimamishwa…
“Sasa?” aliuliza mama Pilima…
“Umefika bado?” aliuliza baba Pili…
“Nikishuka natembea kidogo mpaka kule mbele, lakini hapa panatosha,” alisema mama Pilima, wakaangaliana kwa muda mle ndani ya gari.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Wakasogeleana kama watu waliokuwa wakisikiliza maelekezo ya pamoja. Wakakutanisha midomo, wakaifungua, wakaanza kucheza na denda. Wakawa wanaguna ndani kwa ndani mpaka baba Pili akazima gari…
“Sogeza gari kwa pale mbele basi,” alisema mama Pilima kwa sauti ya kuchoka sana.
Baba Pilima akawasha tena gari, akalisogeza mpaka eneo aliloambiwa na mama Pilima…
“Hapa?”
“Yes! Hakuna mtu anayepita eneo hili muda huu,” alisema mama Pilima hali iliyomfanya baba Pili aamini kwamba huenda wanakwenda kutimiza ndoto yake…
“Egemea kiti,” alisema mama Pilima…


ITAENDELEA

Post a Comment

0 Comments