Recents in Beach

header ads

BABA P...BABA PILI...BABA PILIMA! - 3




Chombezo : Baba P...Baba Pili...Baba Pilima! 
Sehemu Ya Tatu (3)


Baba Pili aliegemea kiti kwa haraka sana, akatumbua macho kusubiri hatua nyingine akiamini ataambiwa au ataelekezwa…
“Mmm! Baba Pili acha mi niende bwana. Muda umekwenda kwelikweli, si ajabu nyumbani wameanza kuingiwa na wasiwasi,” alisema mama Pilima akiwa tayari ameshika kitasa cha mlango ili kushuka…
“Kha! Yaani mbona haifanani?” alihoji baba Pili…http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Nini?”
“Kuniambia nilale mpaka kuaga kwamba unawahi nyumbani…”
“Teh! Teh! Ulidhani nini kitafuata baba Pili? Mbona mimi nimeshaongea mengi na wewe?” alisema mama Pili akiwa ameshafungua mlango wa gari na kushuka.
Mama Pilima alisimama mlangoni, akamwangalia baba Pili kwa sura yenye umakini wa hali ya juu…
“Bai baba Pili, usiku mwema, nafurahia kampani yako,” alisema mama Pilima akaanza kutembea.
Baba Pili akiwa bado ameegemea kiti, alishindwa kujifahamu. Kwa kutumia mwanga hafifu uliokuwa ukitoka kwenye taa za madukani, alimwangalia mama Pilima anavyotembea kuelekea mitaa ya kwake kisha akatingisha kichwa akisema…
“Da! Ameniweza kweli! Yaani kuegemea kiti na kuaga maana yake nini? Yule nadhani kuna kitu ameshtuka, si hivihivi tu.”
Aliwasha gari na kugeuza kurudi kwake.
***
Alipofika nyumbani kwake, mama Pilima alimtumia meseji baba Pili ya kumjulisha amefika salama na kumtakia usiku mwema…
“Nimefika baba Pili, usiku mwema kwako na kwa familia pia, tudumishe upendo wetu.”
“Mh!” aliguna baba Pili.
***
Kulikucha, mama Pilima alikwenda kwenye shughuli zake kama kawaida. Akiwa kwenye pilikapilika alishtuka maeneo f’lani, akaita…
“Baba Pili…baba Pili,” aligeuka mwanaume huyo, akamkazia macho mama Pilima, lakini hakuonesha kumchangamkia.
Mama Pilima alimsogelea huku akiachia tabasamu na kumkazia macho…
“Vipi? Uko sawa baba Pili?” alihoji mama Pilima baada ya kumwona mwanaume huyo akiwa hana uso wa bashasha. Yeye kwa akili zake aliamini hiyo ilisababishwa na kitendo alichomfanyia jana yake, cha kumlaza kwenye kiti cha gari kisha kumwacha…
“Niko sawa, sijakuelewa lakini,” alijibu mwanaume huyo…
“Utanielewa tu baba Pili. Unajua nilishakwambia mimi siwezi kusaliti. Kwa nini usinielewe jamani? Kwani tukiendelea kwa urafiki wetu kuna nini?” alisema mama Pili huku mwanaume huyo akiendelea kumkazia macho…
“Oke, basi tufanye hivi…leo tukutane hotelini, tupeane raha. Lakini iwe leo tu, tusirudie tena. Haya niambie tutakutana saa ngapi na wapi?” alisema mama Pilima na kuuliza swali.
Mwanaume huyo aliwaza sana, akamshangaa mama Pilima lakini hakutaka kumwambia jambo lolote. Ila alimtamani kwa namna mwanamke huyo alivyo mzuri wa umbo mpaka sura. Akaona ile ni bahati ya mtende kwake, kuota jangwani…
“Panga wewe,” alisema…
“Mimi napanga saa kumi, nitakuwa nimemaliza kazi zangu, lakini kuhusu hoteli gani, panga wewe sasa,” alisema mama Pilima.
“Nitakwambia, simu yangu ile nimeiacha, imeharibika kidogo, natumia nyingine hii na namba pia ni nyingine, nitajie upya namba zako,” alisema mwanaume huyo.
Mama Pilima alimtajia namba mwanaume huyo lakini huku akiona kama bado hajachangamka…
“Vipi jana ulifika salama? Nilikutumia meseji hukunijibu. Gari umepaki wapi?” mama Pilima aliuliza maswali mawili kwa mpigo…
“Si ndiyo maana nimekwambia simu ina matatizo kidogo, gari liko kule Mnazi Mmoja kwa mbele.”
Kidogo mwanaume huyo amuulize mama Pilima amsevu kwa jina gani, akashtuka…
“Basi baadaye.”
“Poa baba Pili, utanicheki. Lakini kama nilivyosema, iwe leo tu. Mara moja tu halafu basi, sawa baba Pili?”
“Sawa, nimekuelewa,” alijibu mwanaume huyo akianza kuondoka ili kukwepa maswali zaidi.
Mama Pili alikuwa na mawazo. Aliamini bado hajamridhisha mwanaume huyo kwani hata majibu yake yalionesha hivyo…
“Bado hayuko sawa. Kaniambia ‘basi baadaye’. Angekuwa sawa angeniambia ‘basi baadaye mama Pilima’. Nimemwambia atanicheki, akanijibu sawa, nimekuelewa’. Angekuwa sawa, angenijibu ‘sawa, nimekuelewa mama Pilima’. Nadhani hayupo sawa.”
***
Mbele ya safari, yule mwanaume alimuwaza mama Pilima…
“Kuna wanawake wameumbwa jamani! Yaani yule mwanamke ameumbwa! Nimepata bahati kubwa. Siwezi kumwacha hivihivi tu. Mi amenivutia yale macho yake bwana,” alisema moyoni mwanaume huyo.
***
Saa kumi juu ya alama, mama Pilima alipokea simu kwa namba asiyoijua, akajua ni baba Pili…
“Haloo…niambie baba Pili…wapi? Ooo…napajua…oke… we umeshafika? Haya nakuja sasa hivi mpenzi wangu…”
http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Mama Pilima alichukua usafiri mpaka kwenye hoteli aliyoelekezwa na mwanaume huyo. Akaingia ndani mpaka chumbani bila kupotea ambapo alimkuta mwenyeji wake amejaa tele japo alikuwa hajavua nguo kwa sababu machale yalimcheza…
“Unajua nini…saa zile nakuita pale nilijishtukia, nikasema ni mwenyewe kweli yule…si unajua tena kuonana kwetu ni usiku? Siku ya kwanza usiku, jana usiku, leo ndiyo nimekuona mchana,” alisema mama Pilima huku akikaa kitandani…
“Kweli kabisa…hata mimi mwenyewe sikukujua haraka…” alisema mwanaume huyo akiwa anafunga mlango kwa funguo yeye mwenyewe ili kama kuna mchezo unataka kuchezwa na mwanamke huyo audhibiti mara moja.
“Nilikuona…ulikuwa unanitafuta kwanza kichwani…unajua kukutana baa nako ni shida! Halafu hata sauti yako si ile ya baa…nadhani ile inakuwa ya pombe…kama jana tumezichapa sana,” alisema mama Pilima akiwa anaachia tabasamu…
“Sawa…loo!”
Walikaa kimya kwa muda wakiangaliana kisha mama Pilima akaachia tabasamu la mahaba, akamsogelea mwanaume huyo, akambusu, akamkumbatia, wakakumbatiana. Wakaenda kitandani, puu!
“Baba Pili,” aliita mama Pilima kwa sauti ya chini sana…
“Niambie mpenzi wangu,” alisema mwanaume huyo.
Hapohapo mama Pilima akajiuliza tena ni kwa nini mwanaume huyo hataki kutumia jina la mama Pilima kama alivyozea siku mbili za nyuma?
“Si leo tu lakini?” aliuliza mama Pilima, akimaanisha kwamba, baada ya siku hiyo wasipeane raha tena!
“Sawa, leo tu. Lakini si itategemea?”
Walicheka wote, wakaanza kuhamasishana kwa kushikana sehemu mbalimbali za mwili.
Mara, simu ya mama Pilima iliita lakini ilionekana huyo mtu aliyepiga kama alibip! Kwa hiyo hakuiendekeza, akaendelea na raha zake kitandani.
Walifika mahali wakachojoana ili safari iendelee. Mama Pilima akawa analalamika kwamba ni mara yake ya kwanza kuchepuka…
“Yaani mi leo jamani…yaani sijui itakuaje? Yaani wewe,” alisemasema mama Pilima.
Kazi ikaanza, shughuli ikapamba moto, safari ikakolea, mechi ikachezwa kwenye uwanja binafsi.
Mama Pilima akajikuta akiachana na kulalamikia kuchepuka, akaanza kusikilizia uhodari wa mwanaume huyo na kuzianzisha zile kelele zenyewe sasa.
Ilikuwa fujo, balaa na hekaheka. Ilibidi mwanaume huyo kumziba kinywa mama Pilima ili kelele zake zisiwafaidishe wapangaji wa kwenye vyumba vingine.
Shughuli ilipomalizika, walitulia, wakawa wanahema kwa kasi huku wakipongezana wenyewe kwa wenyewe…
“Hivi baba Pili, tutaweza kweli?” alisema mama Pilima…
“Kuhusu nini?”
“Kwamba baada ya leo na iwe basi?”
“Mh! We unasemaje kwani?”
“Mh! Ngoja tuangalie maana naona umenipa kitu kigeni sana mwilini mwangu. Leo nimesikia kama nabembea kwenye kamba iliyo chini ya mtu mkubwa wenye kutoa kivuli na upepo mwanana toka pwani,” alisema mama Pilima huku akitoka kitandani kuifuata simu yake ambayo ilikazana kuita…
“Sijui atakuwa nani? Labda mume wangu,” alisema kwa sauti mwanamke huyo huku akiishika simu hiyo.
“Hee! Mbona sielewi,” alishtuka. Ni baada ya kuona kwenye skrini jina Baba Pili ambaye yeye aliamini yupo kitandani, akaipokea huku akimwangalia kwa wasiwasi mwanaume huyo kitandani…
“Haloo…”
“Haloo, mama Pilima, mzima?”
“Mi…mzima…hebu subiri na…nakupigia,” alisema mama Pilima na kukata simu, akarudi kitandani…
“Hebu niambie ukweli…wewe siyo baba Pili?” aliuliza mama Pilima huku akionekana kuwa na sura iliyojaa hofu…
“Ni kweli,” alisema mwanaume huyo.
“Imekuaje ukanidanganya sasa?”
“Sijakudanganya, ila wewe uliingia kichwakichwa kwangu. Mimi si baba Pili,” alisema mwanaume huyo kwa sauti yenye unyenyekevu wa hali ya juu.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mama Pilima alichuruzisha machozi, akajiinamia. Akamwangalia mwanaume huyo kwa macho yaliyojaa aibu akiwaza…
“Sasa huyu si amenielewa kuwa mimi ni mwanamke malaya. Lakini ni kwa nini nilimfananisha na baba Pili?”
“Usiumie mpenzi…tunaweza kuendelea na uhusiano…mimi nimekukubali sana. Hata muda ule unaniita, niliamua kuendelea kusimama na kuongea na wewe kwa sababu nilikupenda ghafla palepale, nikaona nimepata bahati ya mtende kuota jangwani,” alisema mwanaume huyo.
Mama Pilima alimwangalia weee, lakini moyoni akakubali kwamba, ni mwanaume mzuri kwake na amemtendea haki. Ina maana akiamua kusema basi, halafu akaendelea na baba Pili atakuwa ameanza tabia ya kurukaruka…
“Kwani wewe kwa jina la mtoto wako yeyote yule unaitwa baba nani?” mama Pilima alimuuliza mwanaume huyo huku akimwangalia kwa macho yaliyojaa mahaba mazito…
“Naitwa baba P.”


“He! Baba P! P ni kifupi au ndiyo jina lote?”
“Kifupi.”
“Kirefu chake?”
“Pilima. Kwa hiyo mimi unaweza kuniita baba Pilima.”
Mama Pilima alicheka sana, akasimama akiendelea kucheka na kusema…
“Haya ni maajabu makubwa kwangu…”
“Kwa nini?”
“Na mimi ni mama Pilima, nina mtoto anaitwa Pilima.”
“Hakuna kitu kama hicho.”
“Kweli kabisa, mtoto wangu anaitwa Pilima.”
“Kwa hiyo mimi mama Pilima, wewe baba Pilima?”
“Ndiyo maana yake.”
Mama Pilima alisahau yote yaliyopita. Alisahau alivyotendwa na mwanaume huyo! Moyoni alisema…
“Kwa hiyo sasa nina baba Pili, baba Pilima feki na baba Pilima orijino yule wa nyumbani.”
***
Uhusiano kati ya mama Pilima na baba Pilima ulipamba moto na kumsahau baba Pili kwa muda. Aliamua kumsahau baba Pili kwa sababu ya kukwepa kukutana naye kimwili wakati ameshajitolea kwa baba Pilima. Angekuwa mwanamke wa ajabu, wanaume watatu kwa wakati mmoja!
Kwa hiyo ikawa kila baba Pili alipompigia simu wakutane, mama Pilima alitoa sababu ya uongo ili kusogeza siku mbele.
Katika kipindi cha wiki mbili, akawa ameshakutana kimapenzi mara mbili na baba Pilima na alikolea kwelikweli. Wao sasa ndiyo walikuwa wakikaa kila jioni kwenye baa nyingine aliyoijua baba Pilima.
Mazungumzo yao walipokaa, mama Pilima alifurahia sana kumwita mwanaume huyo baba Pilima akijisikia kama anamuita mume wake nyumbani…
“Baba Pilima…”http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Niambie mama Pilima…”
“Hivi mapenzi yetu yatadumu kweli baba Pilima?”
“Kwa nini yasidumu mama Pilima, tatizo liko wapi kwani?”
“Sijaona tatizo, bali kama nilivyokwambia, sijazoea kusaliti na nimeshakusimulia mkasa mzima mpaka nilipokutana na wewe.”
“Mimi siwezi kuachana na wewe mama Pilima, kuwa na amani tu.”
Kuna siku, mama Pilima na baba Pilima wakiwa kwenye baa hiyo, mhudumu alijua ni wapenzi kutokana na mikao, kwani uzoefu wake, wanandoa hawakai kihasarahasara, lakini alikuja kushangaa, kumsikia mama Pilima akimuuliza baba Pilima…
“Eti baba Pilima, kwa nini usinywe pombe kali ukaachana na bia?”
“Mama Pilima, pombe kali zinataka watu wanene sana, mimi umbo langu si unaliona?”
“Mh! Kumbe hawa ni mke na mume? Mbona wako kama mtu na hawara yake?” alijiuliza mhudumu huyo baada ya kuwasikia wakiitana majina ya watoto wao.
***
Siku hiyo, akiwa nyumbani, sebuleni na mume wake, mama Pilima alijisahau katika mazungumzo…
“Baba Pilima…eee! Eti baba Pilima,” alikosea mama Pilima, akashtuka, lakini akaendelea kuita jina hilohilo bila mumewe kujua kwamba, hakumaanishwa yeye.
Usiku wa siku hiyo, wakiwa wamelala, baba Pilima alitaka haki yake, akafurukuta akafanikiwa. Lakini wakati mpambano ukiendelea, mama Pilima aliingiza mazoea yaleyale, alimwita mumewe kimahaba…
“Baba Pilima,” lakini alimaanisha yule feki…
“Niambie mke wangu,” aliitika kibabebabe baba Pilima bila kujua kuwa, hakukusudiwa yeye.
***
Ilikuwa Jumapili, mama Pilima alikuwa akijiandaa kwenda kanisani, simu yake ilikuwa mezani sebuleni. Baba Pilima alikuwa hajaamka. Wifi wa mama Pilima alishajiandaa kwa safari ya kanisani, kwa hiyo alikuwa akimsubiri yeye tu. Mara simu ya mama Pilima iliita, wifi yake akaitupia macho…
“Wifi kaka anapiga simu?” alisema wifi mtu huyo baada ya kuona Baba Pilima kwenye skrini ya simu.
Mama Pilima alikwenda mbio…
“Anapigaje wakati bado nipo humuhumu ndani?” aliuliza mama Pilima, akiamini ni kweli mume wake amepiga…
“Ooo! Kumbe huyu!” alisema mama Pilima, wifi yake akachezwa na machale. Kwamba, kwa nini mama Pilima aseme ‘ooo… kumbe huyu’.
Hata hivyo, mama Pilima hakupokea simu hiyo, akaikata na kutuma meseji…
“Ina maana si kaka aliyepiga?” aliuliza wifi huyo…
“Ngoja nitakwambia,” alisema mama Pilima akiwa na uso uliochunwa kwa kukosa aibu. Alijua nini ni nini!
“Mh!” aliguna wifi mtu huyo, lakini akaachana na maswali zaidi.
Ghafla, baba Pilima akatokea kutoka chumbani akiwa ndani ya nguo za kulalia…
“Mbona kama nasikia mimi nimempigia simu mama Pilima wakati sijashika simu yangu tangu kumekucha. Au sijasikia sawasawa?” alihoji baba Pilima huku akipiga miayo.


ITAENDELEA

Post a Comment

0 Comments